

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semindu, Januari 05, 2026, alipokutana na Walimu Wakuu wa shule, Maafisa Elimu pamoja na Watendaji wa Kata, Mitaa na Vijiji.
Mhe. Semindu amewaeleza walimu kutowazuia wazazi na walezi kuwapokea wanafunzi shuleni, huku akiwakumbusha walimu kuwapa wazazi na walezi muda wa kukamilisha mahitaji ya wanafunzi.
“Ifikapo Januari 13, 2026, siku ya kufungua shule, wanafunzi wote wapokelewe bila kujali kama wana sare au hawana sare,” alisisitiza Mhe. Semindu.
Mhe. Semindu ameongeza kuwa lengo la Serikali ni kuboresha miundombinu ya elimu ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata elimu bora.
Aidha, Mhe. Semindu amewasisitiza walimu wanaotekeleza miradi ya maendeleo kuendelea kuongeza jitihada ili kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.
Vilevile, Mhe. Semindu aliwasisitiza walimu kudhibiti utoro wa wanafunzi wawapo shuleni na kuhakikisha wanahudhuria vipindi vyote vya masomo darasani.
Kwa niaba ya walimu
wengine, Magdalena Haali ameahidi kuyatekeleza maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu ili kutimiza lengo la Serikali.
Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.