Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Veronica Kessy ameendelea kutoa Elimu ya kujiandikisha kwenye Daftari la Mpiga ambapo amesema ni haki ya Kikatiba kwa Mwananchi mwenye vigezo vya kujiandikisha ashiriki zoezi hilo linaloendelea hivi sasa na kupiga kura ifikapo Novemba 27,2024.
Mhe. Kessy ametoa elimu hiyo wakati wa Mashindano ya Mpira wa Miguu yaliyofanyika Uwanja wa Mpira Mbulu Mjini kati ya Bargish na Sanubaray, wakati wa kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi la uandikishaji na hatimaye waweze kupiga kura mwezi ujao.
"Niwakumbushe tu kwamba kujiandikisha na kupiga kura ni haki yako ya Kikatiba kwa wewe uliyefikisha miaka 18 na kuendelea, na kuhusu Kitambulisho cha mpiga kura ni kwamba hakihusiki katika uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa bali kitatumika kwenye uchaguzi Mkuu ujao hapo mwakani 2025" Aliongeza Mhe. Kessy.
Katika Mashindano hayo Timu ya Bargish iliibuka mshindi kwa mikwaju ya Penati na kujinyakulia zawadi ya Pesa kiasi cha Shilingi laki 3 huku mshindi namba mbili ambao ni Timu ya Sanubaray wakijipatia zawadi ya Shilingi Laki 2.
Zimesalia siku 4 tangu zoezi la uandikishaji limeanza tarehe 11 Oktoba, 2024 ambapo litahitimishwa tarehe 20 Oktoba, 2024.
Kauli mbiu ni "Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi "
Ujenzi
Anuani: P.O Box 164 Mbulu
Simu: +255 272 2533331
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: td@mbulutc.go.tz
Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.