• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe kwa wafanyakazi |
Halmashauri ya Mji Mbulu
Halmashauri ya Mji Mbulu

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Biashara Viwanda na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Kilimo Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA MANUNUZI
      • FEDHA NA UHASIBU
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UHIFADHI WA MALIASILI NA MAZINGIRA
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
  • Machapisho
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Video
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Matukio
  • Miradi
    • Approved Project
    • Ongoing Project
    • Completed Project
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma kwa watumishi
    • Maij
    • Elimu
    • Uvuvi
  • Kata
    • Ayamaami
    • Ayamohe
    • Bargish
    • Daudi
    • Endagikot
    • Gehandu
    • Gunyoda
    • Imboru
    • Kainam
    • Marangw
    • Murray
    • Nahasey
    • Nambis
    • Sanubaray
    • Silaloda
    • Tlawi
    • Uhuru
  • Uwekezaji
  • Madiwani

MHE. MICHAEL SEMINDU ASISITIZA UHAMASISHAJI WA MAHUDHURIO SHULENI

Posted on: February 20th, 2026



Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Michael Semindu, amewataka watendaji wa kata, vijiji na mitaa pamoja na wataalamu wa sekta mbalimbali kushiriki kikamilifu katika uhamasishaji wa watoto kuripoti shuleni, pamoja na kuchukua hatua madhubuti kudhibiti utoro ili kuhakikisha wanafunzi wanapata haki yao ya elimu.


Akitoa rai hiyo wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) kilichoketi kujadili na kupitia mapendekezo ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027, Mkuu wa Wilaya alisisitiza kuwa usimamizi thabiti wa elimu unahitaji ushirikiano wa karibu kati ya viongozi, wataalamu, wazazi na jamii kwa ujumla.


Alieleza kuwa juhudi za kuongeza mahudhurio shuleni zinapaswa kwenda sambamba na mikakati ya kuboresha mazingira ya kujifunzia, ikiwemo kuhamasisha utoaji wa chakula shuleni na kuimarisha ufuatiliaji wa wanafunzi wanaokosa masomo mara kwa mara.


Katika kikao hicho, wajumbe walijadili kwa kina mapendekezo ya mpango na bajeti, ⁶wakisisitiza umuhimu wa kuhakikisha rasilimali za wilaya zinapangwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi na kuimarisha huduma za msingi kama elimu, afya, maji na miundombinu.


Aidha, wajumbe walikubaliana kuongeza juhudi za uhamasishaji kwa jamii kuhusu umuhimu wa elimu na kuwahimiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanahudhuria shule bila kukosa, huku wakisisitiza ufuatiliaji wa karibu wa utekelezaji wa maamuzi yaliyofikiwa.


Kikao kilihitimishwa kwa maazimio ya kuendelea kuboresha mapendekezo ya mpango na bajeti kabla ya kuwasilishwa katika hatua zinazofuata, kwa lengo la kuhakikisha mipango ya maendeleo ya Wilaya ya Mbulu inaleta matokeo chanya kwa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 July 04, 2025
  • TANGAZO MUHIMU KUTOKA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI KUHUSU MAOMBI YA MPIGA KURA. September 15, 2025
  • TANGAZO LA HUDUMA ZA KIBINGWA KUANZA KUTOLEWA MBULU MJI May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MJI WA MBULU June 09, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • MHE. MICHAEL SEMINDU ASISITIZA UHAMASISHAJI WA MAHUDHURIO SHULENI

    February 20, 2026
  • MADIWANI MBULU TC WAPITISHA BAJETI YA 2026/2027 YA TSH BILIONI 33.2

    February 19, 2026
  • FANYENI MAANDALIZI YA MATIBABU KABLA YA KUKUMBWA NA CHANGAMOTO

    February 17, 2026
  • ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WANANCHI WA MTAA WA HAYAHAYA-AYAMAAMI

    February 16, 2026
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN BUNGENI
More Videos

Tovuti mashuhuri

  • Babati dc Website
  • Hanang' dc Website
  • Babati Town Website
  • Simanjiro Website
  • Kiteto Website
  • Mbuludc Website

Tovuti Mbadala

  • Tamisemi
  • Ikulu
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • Mbulu Tc Facebook
  • Mbulu Town Council WatsApp
  • Mbulu Tc Instagram

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.