• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe kwa wafanyakazi |
Halmashauri ya Mji Mbulu
Halmashauri ya Mji Mbulu

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Biashara Viwanda na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Kilimo Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA MANUNUZI
      • FEDHA NA UHASIBU
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UHIFADHI WA MALIASILI NA MAZINGIRA
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
  • Machapisho
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Video
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Matukio
  • Miradi
    • Approved Project
    • Ongoing Project
    • Completed Project
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma kwa watumishi
    • Maij
    • Elimu
    • Uvuvi
  • Kata
    • Ayamaami
    • Ayamohe
    • Bargish
    • Daudi
    • Endagikot
    • Gehandu
    • Gunyoda
    • Imboru
    • Kainam
    • Marangw
    • Murray
    • Nahasey
    • Nambis
    • Sanubaray
    • Silaloda
    • Tlawi
    • Uhuru
  • Uwekezaji
  • Madiwani

FANYENI MAANDALIZI YA MATIBABU KABLA YA KUKUMBWA NA CHANGAMOTO

Posted on: February 17th, 2026


Wananchi wa Kijiji cha Tsaayo wamehimizwa kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote kama hatua ya mapema ya kujikinga na changamoto za kiafya na kulinda uchumi wa familia zao.


Rai hiyo imetolewa leo, Februari 17, 2026, wakati wa zoezi la utoaji wa elimu ya bima ya afya lililofanyika kijijini hapo, likiwalenga makundi mbalimbali ya jamii.


Akizungumza katika mkutano huo, Mratibu wa Bima ya Afya, Dkt. Basil Manda, amesema kujiunga mapema na bima ya afya kunapunguza athari za kifedha zinazotokana na magonjwa ya ghafla na ni kinga muhimu ya maisha.


Ameongeza kuwa serikali inaendelea kuboresha huduma za afya na kusogeza huduma karibu na wananchi, hivyo wananchi wanapaswa kutumia fursa hiyo kwa kujiunga na bima.


Dkt. Manda amesisitiza kuwa mpango huo una faida nyingi ikiwemo kupata huduma katika vituo vilivyosajiliwa, kupunguza ucheleweshaji wa matibabu na kuongeza uhakika wa huduma kwa familia.


Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Ndugu Tomic Simbeye, amesema afya bora ni msingi wa maendeleo na kujiunga na bima ni njia ya kujilinda dhidi ya gharama zisizotarajiwa za matibabu.


Amehimiza wazazi kuhakikisha wanawaandikisha watoto wao ili kulinda ustawi wa familia na mustakabali wao wa kiafya.


Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Tsaayo, Ndugu Silvin Bura, amewashukuru wataalamu kwa kutoa elimu hiyo na kuhimiza wananchi kujiunga kwa wingi na mpango wa bima ya afya.


Wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali na kupewa ufafanuzi kuhusu taratibu za kujiunga, uchangiaji na matumizi ya huduma za bima.


Utoaji wa elimu ya bima ya afya unaendelea katika maeneo mbalimbali ili kuongeza usajili wa wananchi na kuimarisha huduma za afya ngazi ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 July 04, 2025
  • TANGAZO MUHIMU KUTOKA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI KUHUSU MAOMBI YA MPIGA KURA. September 15, 2025
  • TANGAZO LA HUDUMA ZA KIBINGWA KUANZA KUTOLEWA MBULU MJI May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MJI WA MBULU June 09, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • FANYENI MAANDALIZI YA MATIBABU KABLA YA KUKUMBWA NA CHANGAMOTO

    February 17, 2026
  • ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WANANCHI WA MTAA WA HAYAHAYA-AYAMAAMI

    February 16, 2026
  • VIJANA WAHIMIZWA KUFANYA KAZI KWA BIDII NA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO

    February 14, 2026
  • ELIMU YA BIMA YA AFYA YA TOLEWA KWA WANANCHI WA ENDAMAKSI NA MAHERI

    February 14, 2026
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN BUNGENI
More Videos

Tovuti mashuhuri

  • Babati dc Website
  • Hanang' dc Website
  • Babati Town Website
  • Simanjiro Website
  • Kiteto Website
  • Mbuludc Website

Tovuti Mbadala

  • Tamisemi
  • Ikulu
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • Mbulu Tc Facebook
  • Mbulu Town Council WatsApp
  • Mbulu Tc Instagram

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.