• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe kwa wafanyakazi |
Halmashauri ya Mji Mbulu
Halmashauri ya Mji Mbulu

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Mbulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Biashara Viwanda na Uwekezaji
      • Mipango na Uratibu
      • Kilimo Mifugo na Uvuvi
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Miundombinu na Maendeleo ya Vijiji na Miji
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • UKAGUZI WA NDANI
      • USIMAMIZI WA MANUNUZI
      • FEDHA NA UHASIBU
      • MAWASILIANO SERIKALINI
      • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
      • HUDUMA ZA SHERIA
      • UHIFADHI WA MALIASILI NA MAZINGIRA
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
  • Machapisho
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Video
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Matukio
  • Miradi
    • Approved Project
    • Ongoing Project
    • Completed Project
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma kwa watumishi
    • Maij
    • Elimu
    • Uvuvi
  • Kata
    • Ayamaami
    • Ayamohe
    • Bargish
    • Daudi
    • Endagikot
    • Gehandu
    • Gunyoda
    • Imboru
    • Kainam
    • Marangw
    • Murray
    • Nahasey
    • Nambis
    • Sanubaray
    • Silaloda
    • Tlawi
    • Uhuru
  • Uwekezaji
  • Madiwani

TAMISEMI yaandaa mwongozo mpya wa usimamizi wa mapato kwa Halmashauri

Posted on: July 11th, 2018

Serikali imesema kuwa mwongozo mpya wa ukusanyaji mapato katika halmashauri unalenga kuongeza wigo wa makusanyo ya mapato kwa kuwatoza watu wengi badala ya wachache na hivyo kuziwezesha halmashauri kukusanya mapato mengi zaidi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mratibu wa Mradi wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Bi Beatrice Njawa mara baada ya ufunguzi wa kikao cha kujadili Mwongozo wa Usimamizi Ukusanyaji Mapato katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ndogo ya TAMISEMI iliyopo jijini Dar es salaam.

Alieleza kuwa mwongozo wa usimamizi wa mapato utapanua wigo kwa kuwatoza wale wote wanaostahili kutozwa mapato mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushuru na kodi mbalimbali za Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Bi Njawa aliongeza kuwa mwongozo mpya sambamba na kuongeza wigo wa ukusanyaji mapato ya halmashauri umezingatia kushirikisha maoni ya wadau hususani sekta binafsi ili waweze kutoa elimu kwa wadau wao wa namna bora ya kuutekeleza mwongozo huo ili kufikisha malengo yaliyokusudiwa.

“Kupitia mwongozo huu tumeshirikisha sekta binafsi ambao watatusaidia kutambua baadhi ya  shughuli za kiuchumi zilizopo katika maeneo yao ili tuweze kuibua vyanzo vipya isipokuwa kwa tahadhari kwamba havitakuwa kero katika jamii ya wafanya biashara.

Mapema akifungua kikao hicho kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es salaam bwana Abubakar Mussa Kunenge alisema kuwa Mwongozo huo ni jitihada za Serikali za kuziwezesha Halmashauri kukusanya Mapato ya Vyanzo vya Ndani kwa ufanisi na kikamilifu. Kadhalika, kuweka mikakati ya kuwezesha kuwepo kwa mazingira wezeshi ya kufanya biashara na uwekezaji.

Aliongeza kuwa mwongozo huo unalenga kuweka utaratibu rahisi wa utambuzi wa Fursa za kiuchumi na Sekta ya uzalishaji, utambuzi wa Walipa kodi, taarifa na takwimu za kodi, namna ya kusimamia na kukusanya mapato, ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika mipango na utekelezaji wa mikakati ya ukusanyaji mapato, kuongeza uwajibikaji na uwazi katika kukusanya na kutumia mapato yaliyokusanywa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais TAMISEMI Bwana Shomari Mukhandi alisema kuwa Ofisi yake imeona ni vyema kukaa na wadau kujadili rasimu ya mwongozo huo ili kupata maoni ya kila mshiriki ili kuboresha Mwongozo wa Ukusanyaji Mapato kulingana na mahitaji ya Sekta mbalimbali za Kiuchumi na Kijamii kwa kuzingatia kuimarisha Uwazi, Uwajibikaji na Ukuzaji  Uchumi.

Naye bwana Donald Ria ambaye ni Mtaalamu Mshauri wa masuala ya mazingira ya biashara na uwekezaji kutoka Mradi wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Denmark na Tanzania alisema kuwa mradi wake ulikubali kufadhili kuandaliwa kwa mwongozo huo ili kuboresha ukusanyaji wa mapato katika halmashauri.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 July 04, 2025
  • TANGAZO LA HUDUMA ZA KIBINGWA KUANZA KUTOLEWA MBULU MJI May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MJI WA MBULU June 09, 2025
  • KAMPENI YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMINI A NA UPIMAJI WA HALI YA AFYA KWA MTOTO June 01, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • WATAALAMU WA AFYA WAMETAKIWA KUZINGATIA TARATIBU KUWAHUDUMIA WATOTO NJITI.

    July 29, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2O25 WARIDHISHWA NA MRADI WA JENGO LA MAMA NA MTOTO MBULU TC

    July 16, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 KUTEMBELEA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 44.3 WILAYANI MBULU

    July 16, 2025
  • WANANCHI WASISITIZWA KUWA MSTARI WA MBELE UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU.

    July 10, 2025
  • Ona zote

Video

HOTUBA YA MHE. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN BUNGENI
More Videos

Tovuti mashuhuri

  • Babati dc Website
  • Hanang' dc Website
  • Babati Town Website
  • Simanjiro Website
  • Kiteto Website
  • Mbuludc Website

Tovuti Mbadala

  • Manyara Reginal Website
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Ikulu
  • BLOG RASMI YA OFISI YA WAZIRI MKUU
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.