Halmashauri 33 kati ya halmashauri 185 zimeweza kukusanya mapatoya ndani kwa kiwango cha asilimia 50 na zaidi ya makisio ya mwaka wa fedha2018/19 huku halmashauri 21 zikiwa zimefanya vibaya kwa kusanya chini yaasilimi 20 ya makisio yake kwa mwaka.
Hayoyamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali zaMitaa Mhe. Selemeni Jafo alipokuwa akitoa taarifa ya mapato ya ndani yahalmashauri kwa robo ya pili ya mwaka.
Alisemakatika Halmashauri 33 zilizokusanya asilimia 50 na zaidi zimo Halmashauri za Majiji tatu zikiongozwa na Jiji la Dodoma, Manispaa ni mbili zikiongozwana manispaa ya Iringa, Halmashauri za Miji nane zikizongozwa na Mji wa Geita naHalmashauri za Wilaya ni ishirini zikiongozwa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita.
“Uchambuziunaonyesha kuwa Katika Majiji 6, Jiji la Dodoma linaongoza kwa kukusanyaasilimia 59 ya makisio na Jiji la Tanga limekuwa la mwisho kwa kukusanyaasilimia 33 ya makisio” alisema.
AidhaManispaa ya Iringa imeongoza katika kundi la Manispaa kwa kukusanya asilimia 64ya makisio ambapo Manispaa ya Lindi imekuwa ya mwisho katika kundi hili kwakukusanya asilimia 20 ya makisio.
Jafoaliongeza kuwa kwa upande wa Halmashauri za Miji, Halmashauri ya Mji wa Geitaimeongoza kwa kukusanya asilimia 84 ya makisio na Halmashauri ya Mji waNanyamba imekuwa ya mwisho katika kundi hili kwa kukusanya asilimia 9 tu yamakisio,
AlisemaKatika kundi la Halmashauri za Wilaya, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeongozakwa kukusanya asilimia 78 ya makisio ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbuimekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 6 tu ya makisio.
Kwakuzingatia wingi wa makusanyo ya mapato ya Halmashauri Jafo alibainishaHalmashauri iliyoongoza kwa kuwa ni Jiji la Dodoma ambalo limekusanya ShilingiBilioni 40.12 na halmashauri iliyokusanya kiasi kidogo cha fedha ni halmashauriya Wilaya ya Momba ambayo imekusanya shilingi milioni 105.04.
WaziriJafo pia alibainisha Mkoa ambao Halmashauri zake zimekusanya mapato kwakuzingatia wingi wa mapato kuwa ni Mkoa wa Dar es salaam ambao kwa jumlahalmashauri zake zimekusanya shilingi bilioni 77.4 na Mkoa wa Mwisho ni Kataviambao halmashauri zake zimekusanya shilingi bilioni 2.4 tu.
Alisemakatika Mkoa uliokusanya vizuri kwa kuzingatia asilimia ya makusanyo ni Mkoa wa Geita Halmashauri zake zimekusanya asilimia 56.4 ya makisioya mwaka ukifuatiwa kwa karibu na Mkoa wa Dodoma uliokusanya asilimia 55.9 yamakisio yake na Mkoa wa mwisho kwa kigezo hicho ni Mkoa wa Mtwara ambaoumekusanya asilimia 15 ya makisio yake ya mwaka.
Wakatihuo huo Waziri Jafo amewataka wakurugenzi wote ambao Halmashauri zaohazikufanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato kwa kukusanya chini ya asilimiakumi ya makisio yake kwa kipindi cha nusu mwaka kujieleza na kujitathimini nakuhakikisha wanaongeza bidii katika suala la ukusanyaji wa mapato.
“Halmashauri9 kati ya 10 zilizofanya vibaya katika mwaka wa fedha uliopita zimefanikiwakufanya vizuri katika kipindi cha nusu mwaka wa fedha 2018/19 kwa kukusanyazaidi ya asilimia 20 ya makisio yake” alisema .
WaziriJafo pia aliwaagiza Wakurugenzi wote kuhakikisha takwimu zote za mapato katikamfumo wa LGRCIS zinafanyiwa usuluhisho na kutumwa katika mfumo wa IFMS(Epicor) kwani taarifa zote za mapato na matumizi ya fedha zinatakiwa kutolewakupitia mfumo huo.
Ulinganifuhuu wa taarifa za mapato umelenga kuonesha jinsi kazi za ukusanyaji wa mapatoya ndani katika Mamlaka za Serikali za Mitaa inavyoendelea kusimamiwa vyema natakwimu hizi zinazotolewa ni kwa mujibu wa taarifa zilizofanywiwa usuluhisho nakutumwa katika mfumo wa IFMS(Epicor).
Katikamwaka wa fedha 2018/19 Halmashaurti zilipangiwa kukusanya shilingi bilioni735.6 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani na hadi kufikia Disemba 31,2018Halmashauri zimekusanya shilingi bilioni 300 sawa na asilimia 41 ya makisio.
Kwakipindi cha kwa mwaka 2017/18 halmashauri zilipanga kukusanya shilingi bilioni687.3 na hadi kufikia Disemba,2017 halmashauri hizo zilikuwa zimekusanya sh bilioni 281.3 sawa na asilimia 41 ya makisio.
Takwimuhizi zinabainisha kuwa kuna ongezeko la Shilingi bilioni 18.7 kwa mwaka wafedha 2018/19 ikilinganishwa na makusanyo kwa kipindi kama hiki kwa mwaka wafedha 2017/18.
Ujenzi
Anuani: P.O Box 164 Mbulu
Simu: +255 272 2533331
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: td@mbulutc.go.tz
Copyright ©2020 GWF . All rights reserved.